Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake
Chadema (Bawacha) na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee alikosa
dhamana na kupelekwa rumande katika Gereza la Segerea.
Mdee pamoja na wenzake wanane, walifikishwa katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka mawili
likiwamo la kutotii amri halali ya Jeshi la Polisi na kufanya mkusanyiko
usio halali.
Mdee akitoka ndani ya Makakama na kusalimia raia
Halima Mdee (Mwenye suti nyeusi) na wafuasi wengine wa Chadema
wakisindikizwa kupanda gari la polisi baada ya kutokamilika kwa dhamana
yao katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Dar es salaam.
Mhe, Othman Masoud Othman
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein, amefanya Uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serekali ya Mapinduzi
Zanzibar, kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu 55(1)cha Katiba
ya Zanzibar ya 1984.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi amemteuwa Mhe,
Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Uteuzi huo umeaza
leo 7,Oktoba 2014. Kabla ya uteuzi huo Mhe, Said Hassan Said alikuwa
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mhe, Said Hassan Said, anachukua nafasi ya aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Mhe, Othman Masoud Othman ambaye uteuzi wake umefutwa kwa
mujibu wa Vifungu vya 53,54 (1) na 55(3) vya Katiba ya Zanzibar ya 1984
na kifungu 12 (3) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Namba 2 ya 2011.
Rais
wa Kenya, Uhuru Kenyatta, amefika mbele ya mahakama ya kimataifa ya
uhalifu ICC huko Hague, ambako anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu dhidi
ya binaadamu.
Yeye ni kiongozi wa kwanza wa taifa kuwasili mbele ya mahakama hiyo.
Kenyatta
amefika mbele ya mahakama hiyo baada ya waendesha mashtaka kuishutumu
serikali ya Kenya kukata kuwasilisha ushahidi muhimu.
Kenyatta
amekanusha madai ya kupanga na kufadhili ghasia za kikabila nchini Kenya
baada ya uchaguzi uliokumbwa na utata mwaka 2007/2008.
Kikao cha
leo kitatathmini ombi la upande wa mashitaka la kutaka kuahirishwa kwa
kesi hiyo hadi pale serikali ya Kenya itakapoikabidhi mahakama hiyo
ushahidi unaohitajika kuhusiana na mali ya Rais Kenyatta.
Upande
wa utetezi nao unataka kesi hiyo ifutiliwe mbali ukisema kuwa upande wa
mashitaka hauna ushahidi wa kutosha kwa kesi hiyo kuendelea.
Kiongozi wa mashitaka Fatou Bensouda, amewasili mahakamani akisema kesi hiyo iko katika awamu muhimu sana.
Kenyatta ameamua kukaa kimya akimtaka wakili wake kuongea kwa niaba yake.
Mtu
wa kwanza aliyeugua ugonjwa wa Ebola nchini Marekani amefariki
,hayo ni kwa mujibu wa maafisa wa afya katika hospitali ya Texas.
Thomas
Eric Duncan mwenye picha hapo juu aliambukizwa Ebola huko nchini Liberia
,alikuwa amewekwa katika karantini katika hospitali moja ya mjini Dallas
ili kupewa dawa za majaribio.
Awali ,Marekani ilitangaza masharti
mapya ya usalama katika viingilio vyote vya taifa hilo ili kuwakagua
wasafiri walio na dalili za ugonjwa huo.
Zaidi ya watu 3000
wamefariki na wengine 7500 kuambukizwa wengi wao kutoka Afrika Magharibi
katika mlipuko mbaya wa ugonjwa wa Ebola.
Huku Dancun akiwa raia
wa kwanza nchini Marekani kupatikana na ugonjwa huo,raia watatu wa
Marekani pamoja na mpiga picha mmoja waliambukizwa virusi vya ugonjwa
huo nchini Liberia.
Habari hizo zilijiri mda mchache tu baada ya
waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani John Kerry kutoa wito kwa
mataifa yote kuimarisha juhudi zao za kukabiliana na ugonjwa huo.
Mkuu wa Idara ya Usalama nchini
Marekani, aliyekuwa na jukumu la kumlinda Rais Barack Obama, amejiuzulu
kufuatia matukio yenye kuhatarisha usalama wa taifa yaliyotokea.
Mkuu huyo wa usalama Julia Pierson alikabidhi barua ya kujiuzulu kwa Waziri wa Usalama wa Ndani, Jumatano.
Siku
moja kabla, alikabiliana na maswali ya wajumbe wenye hasira kutoka
Baraza la Congress juu ya udhaifu mkubwa wa usalama wa Ikulu ya Marekani
Habari
za tukio lingine likimhusisha mtu mwenye silaha kuruhusiwa kuingia
katika lifti moja na Bwana Obama kulizidisha kutolewa wito wa kumtaka
mkuu wa usalama kujiuzulu.
"Leo, Julia Pierson, mkurugenzi wa
usalama wa taifa wa Marekani, amenikabidhi barua ya kujiuzulu, na
nimeikubali," Waziri wa Usalama wa Taifa Jeh Johnson aliandika katika
taarifa.
"Nampongeza kwa utumishi wake wa miaka 30 katika idara ya usalama na taifa."