Pages

Monday, 22 August 2016

Utafiti:Madaktari Kusini mwa Sahara huzidisha dawa kwa wagonjwa

Image caption





Inasemekana tatizo ni baya zaidi kwenye taasisi zinazotengeneza faida, na kuchochea kuuza dawa
Utafiti unaonyesha kuwa madaktari wa nchi za kusini mwa Afrika wanatoa dawa nyingi zaidi ya zilizoagizwa na Shirika la Afya Duniani WHO.
Utafiti huo uliofanywa na Chuo kikuu cha London kwa ushirikiano na kituo cha Kutoa ushauri wa afya cha nchini Ghana,ikihusisha nchi kumi na moja za kusini mwa jangwa la Sahara zinaonyesha kuwa wagonjwa wanapewa takribani dawa tatu kila wanapotembelea hospitali, moja zaidi ya maelekezo ya WHO.
Inasemekana tatizo ni baya zaidi kwenye taasisi zinazotengeneza faida, na kuchochea kuuza dawa.
Image caption



Wagonjwa wengi wamekuwa wakipewa dawa za kutuliza maumivu pasipo kufanyiwa vipimo
Tafiti zimeonya kuwa matumizi makubwa ya madawa yanasababishwa na kulazimishwa kutumia dawa, kuzidisha dozi na kuleta athari mbaya kwa mchanganyiko unaosababishwa na kuchanganya dawa mbalimbali.
Pia wamegundua wagonjwa wengi wamekuwa wakipewa dawa za kutuliza maumivu pasipo kufanyiwa vipimo, na kuongeza hatari ya maambukizo yanayosababisha na kupambana na dawa.
#BBC SWAHILI.

Saturday, 20 August 2016

SIMBA WABAMIZA NDANDA FC 3-1

Mshambuliaji wa Timu ya Simba, Shiza Kichuya akiachia shuti lililopelekea kuipatia Timu yake bao la tatu dhidi ya Timu ya Ndanda, katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania uliochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda Bao 3-1.
Mshambuliaji wa Timu ya Simba, Shiza Kichuya akishangilia Ushindi sambamba na Mashabiki wa Simba baada ya kuipatia timu yake bao la tatu dhidi ya Timu ya Ndanda, katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania uliochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda Bao 3-1.
 Mshambiaji wa Simba, Laudit Mavugo akiondoka na kijiji cha wachezaji wa Ndanda katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania uliochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda Bao 3-1.
Kipa wa Simba, Vincent Agban akiruka na kuusindikiza kwa macho mpira ukiingia wavuni baada ya kupigwa kichwa safi kabisa na Mshambuliaji wa Timu ya Ndanda, Omary Mponda na ikiwa ni goli la kufutia machozi katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania uliochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda Bao 3-1.
Beki wa Simba, Mohamed Hussein akiondoka na mpira.

JESHI LA POLISI WAKIWA KATIKA MAZOEZI YA UTAYARI WA KUKABILIANA NA MATUKIO NA VITENDO VYA UHALIFU NA WAHALIFU NCHINI.



Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wa wakiwa moja ya maozezi yao ya kupasha viungo kabla ya kuanza mazoezi ya kutuliza ghasia.
Askari Polisi wa kikosi maalum cha polisi (CRT) wa mkoa wa Iringa wakiwa katika mazoezi ya utayari wa kukabiliana na matukio yoyote yatakayojitokeza katika maeneo mbalimbali.
Askari wa vikosi vya kutuliza ghasia wa mikoa mbalimbali wakiwa na magari yao wakati wa mazoezi ya utayari wa kupambana na matukio mbalimbali ya uhalifu na wahalifu katika maeneo mbalimbali.
Askari wa vikosi vya kutuliza ghasia wa wakiwa na magari yao wakati wa mazoezi ya utayari wa kutuliza ghasia na kukabiliana na matukio yoyote ya uhalifu na wahalifu.
Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoa wa Lindi wakifanya mazoezi magumu ya kijiweka tayari kukabiliana na matukio yoyote yatakayojitokeza ikiwemo watu wasiotii amri za Jeshi la Polisi ikiwa ni pamoja na kutofuata sheria za nchi.
Askari Polisi wa vikosi vya kutuliza ghasia wa wa mikoa ya Lindi, Iringa, kanda maalumu ya Dar es salaam na mikoa mengine wakipokea maelekezo mbalimbali wakati wa mazoezi ya tayari katika kukabiliana na matukio mbalimbali ya uhalifu na wahalifu (Picha zote na makao makuu ya Jeshi la Polisi.)

MAGAZETI YA JUMAMOSI 20, AGOSTI 2016.