Pages

Thursday 25 December 2014

Shangwetz blog tunawatakia kheri ya Chrismass na mwaka mpya 2015.

Blog ya Jamii Shangwetz inawatakia kheri na nafaka kwa chrismass na mwaka mpya 2015.
Tusherekee kwa amani na utulivu ili tuzidi kudumisha amani na usalama katika taifa letu na tuendelee kufungua blog hii kwa habari na matukio motomoto.
Mungu bariki Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla.

Picha 6 Diamond akiwa na Jk Ikulu Jijini Dar es salaam hivi karibuni

Rais Dkt Jakaya Kikwete amkaribisha Ikulu msanii wa mziki wa Bongo fleva Naseeb Abdul maarufu kama"Diamond" nakuwapongeza na Idris Sultan mshindi wa Big brother Africa kwa kuletea sifa Taifa letu mwaka huu 2014.

Rais alimpongeza Diamond kwa kushinda tuzo tano za muziki za kimataifa mwaka huu 2014 alipokaribishwa Ikulu na kwa na mazungumzo na Naseeb.

Katika hatua hiyo Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete alipata maelezo toka kwa msanii Naseeb Abdul "Diamond" wakati akionyesha tuzo tano za muziki za kimataifa alizoshinda mwaka huu 2014 sambamba na kumuelezea jinsi alivyoshinda tuzo hizo.

Baada ya kuongea nae kwa mda Diamond alimkabidhi Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete CD mpya ya wimbo wake unaotamba kwa sasa.

Hizi ni miongoni mwa picha 6  Jk akiwa na Diamond.














Wednesday 24 December 2014

Gari linalojiegesha lenyewe dereva akishuka

Kampuni ya BMW imezindua kifaa ambacho kinawezesha gari lako kujiegesha lenyewe
Hakuna kitu kibaya kama kusahau ulikoegesha gari lako katika jengo la kuegeshea magari lenye gorof nyingi.
Lakini hivi karibuni hautahihajika kupanda gorofa kutafuta gari lako kwani kampuni ya kutengeza magari ya BMW, imetangaza kuzundia kifuaa ambacho kinaweza kuyawezesha magari ya kampuni hio kujiegesha yenyewe kwa kubonyeza tu kifaa hicho.
Hata hivyo dereva wa gari hilo atalazimika kuvaa saa ya Smartphone mkononi ambayo ataibonyeza na kuiamrisha kwa sauti gari hilo kwenda kujiegesha.
Gari hili linaweza kujiegesha lenyewe kwa kutumia saa ya mkononi ambayo inabonyezwa na dereva
Gari hilo kwa amri ya dereva litatoka liliko baada ya dereva kushuka na kwenda lenyewe kwa kuhesabu muda utakaolichukua kwenda kutafuta sehemu ya kujiegesha.
Tawi la kampuni ya BMW mjini Munich, Ujerumani limezindua teknolojia hio ambayo inawezesha gari kujiegesha lenyewe.
Gari hilo linatumia miale ya Leser iliyo kujitafutia ramani ya jengo ambalo lipo. Dereva anaweza kuliamrisha gari hilo kwenda kujiegesha kwa kutumia Smartphone.
Dereva anaporejea kutoka alikokwenda, analiamrisha gari kutoka sehemu ilikojiegesha na kuja kumchukua dereva
Teknolojia hio inajulikana kama ' Remote Valet Parking Assistant,' na inafanyiwa majaribio kwenye gari la BMW i3.
Badala ya kutumia GPS, teknolojia hio inatumia miale ya Laser ambayo hutengeza ramani inayolisaidia gari hilo kutafuta sehemu ya kwenda kujiegesha.
Teknolojia hiyo inaiwezesha gari hilo kuona njia na nafasi ya kujiegeshea na pia kuona vizingiti mfano kama magari ambayo hayajaegeshwa vyema.
Kwa mujibu wa waliotengeza gari hilo, linaweza kujitafutia nafasi ya kujiegesha na hata kuweza kutambua sehemu ambako kuna nafasi.
Teknolojia hio inatengezwa sambamba na teknolojia nyinginezo zitakazoweza kuzuia gari hilo kugongana na magari mangeine.
 mkononi ambayo ataibonyeza na kuiamrisha kwa sauti gari hilo kwenda kujiegesha.
Gari hili linaweza kujiegesha lenyewe kwa kutumia saa ya mkononi ambayo inabonyezwa na dereva
Gari hilo kwa amri ya dereva litatoka liliko baada ya dereva kushuka na kwenda lenyewe kwa kuhesabu muda utakalichukua kwenda kutafuta sehemu ya kujiegesha.
Tawi la kampuni ya BMW mjini Munich, Ujerumani limezindua teknolojia hio ambayo inawezesha gari kujiegesha lenyewe.
Gari hilo linatumia miale ya Leser iliyo kujitafutia ramani ya jengo ambalo lipo. Dereva anaweza kuliamrisha gari hilo kwenda kujiegesha kwa kutumia Smartphone.
Dereva anaporejea kutoka alikokwenda, analiamrisha gari kutoka sehemu ilikojiegesha na kuja kumchukua dereva
Teknolojia hio inajulikana kama ' Remote Valet Parking Assistant,' na inafanyiwa majaribio kwenye gari la BMW i3.
Badala ya kutumia GPS, teknolojia hio inatumia miale ya Laser ambayo hutengeza ramani inayolisaidia gari hilo kutafuta sehemu ya kwenda kujiegesha.
Teknolojia hiyo inaiwezesha gari hilo kuona njia na nafasi ya kujiegeshea na pia kuona vizingiti mfano kama magari ambayo hayajaegeshwa vyema.
Kwa mujibi wa waliotengeza gari hilo, linaweza kujitafutia nafasi ya kujiegesha na hata kuweza kutambua sehemu aambako kuna nafasi.
Teknolojia hio inatengezwa sambamba na teknolojia nyinginezo zitakazoweza kuzuia gari hilo kugongana na magari mangeine.

Monday 22 December 2014

Mliokosa hotuba ya Rais Jk hii hapa....

HOTUBA YA MH RAIS

Kikwete: Naendelea kuimarika kila siku japo sipo fit kabisa. Leo nazungumzia uchaguzi wa serikali za mitaa, umeenda vizuri ukiacha maeneo machache. Ni uthibibitisho wa kuendelea na kukomaa kwa demokrasia na natoa pongezi kwa walioshinda na wakae chini kupanga mikakati ya kuongoza maeneo yao. Katika taarifa ya waziri Ghasia alielezea kasoro zilizojitokeza na aliahidi kuchukua hatua. Nieleze furaha yangu kwa Hawa Ghasia juu ya hatua alizochukua na mimi nikaweka ridhaa yangu, lazima watumishi wajue kuna adhabu ya makosa wanayoyafanya, kuwawajibisha itakua fundisho kwao na kwa wengine wawe makini kwenye uchaguzi wa 2015.

Jambo la pili ni sakata la Tegeta escrow, wakati wa bunge la bajeti kulitokea madai kuwa fedha za escrow zilizokuwa benki kuu zimechotwa kinyemela na PAP kwa kushirikiana na viongozi wa serikali. Serikali iliahidi kutekeleza kwa kupitia kwa CAG kufanya ukaguzi ambayo ilisomwa bungeni pia niliagiza kuchapishwa kwenye magazeti na tovuti ya serikali, TAKUKURU wanaendelea na uchunguzi wao, taarifa yao ni kuwaona mahakamani, hawana ya maelezo. Tarehe 8 Desemba nilipoanza kazi, niliyasoma na kutoa maagizo, zipo taarifa nilizozipata japo sio zote, lakini nilisema siwezi kusubiri sana. Katika kusoma makaratasi na kupewa maelekezo, yapo mambo manne mikataba ya umeme, umiliki wa PAP, kodi ya serikali na tuhuma za rushwa.

Mikataba ya kununua umeme unaozalishwa na makampuni binafsi, mikataba ya umeme iko ya namna mbili tozo ya umeme ikiwa ni malipo ya umeme uliotumiwa kulingana na bei waliyokubaliana na ya pili ni gharama ya uwekezaji(capacty charge) kwa Songas, Aggreko, IPTL

Anaelezea historia ya mgogoro wa TANESCO na IPTL, TANESCO na IPTL walikubaliana kuanzisha akaunti ya Tegeta escrow benki kuu na kuingia mkataba, wizara ya madini kwa niaba ya TANESCO na IPTL na benki kuu kama wakala. Masharti ilikua kampuni ya IPTL itaendelea kupeleka madai yake TANESCO ya tozo ya uwekezaji na TANESCO itaendelea kulipa lakini yataenda escrow akaunti badala ya IPTL lakini ya umeme yaliendelea kwenda IPTL na ilifunguliwa 2006 na mpaka kesi kuamuliwa 2013 wakati IPTL inachukuliwa na PAP walikua hawajamalizana. (They decided to manage the crisis rather than resolve it)

Kwa mujibu wa mkataba, TANESCO isipolipa inatozwa riba ya 2%, kwa mujibu wa taarifa akaunti ilikua na 202.9 bilioni na sio 309.7, hizi zilipaswa kuwepo endapo TANESCO ingelipa zote kwa wakati. 

Fedha hizi mwenyewe nani, umma au IPTL
Nianze kuelezea ya Escrow ni kitu gani, ni tofauti kidogo na akauti zetu tatu tulizozizoea, na akauti maalumu na kazi maalumu pia ikiisha na yenyewe inafungwa, inasimamia na wakala na wakala pia anajukumu la kumlipa mwenye fedha wakati ukifika.

Akaunti ikafunguliwa BoT kwa ajili ya kuweka tozo ya uwekezaji, zinahifadhiwa ili kutoa nafasi kwa pande mbili kushughulikia tofauti zao lakini kabla ya hapo TANESCO walikua wanalipa moja kwa moja. 

Kimsingi fedha hizi ni za IPTL, katika swali pesa za nani, mdhibiti wa hesabu alisema humu yawezekana zipo za umma pia zipo za IPTL, Nilipomuuliza maana, akasema zamani walikua wanalipa moja kwa moja lakini baada ya mzozo walikubaliana kwanza waziweke BoT. 

Kama mgogoro ungetatuliwa na madai ya TANESCO yakakubali ya tozo kupunguzwa, kiasi kilichopunguzwa kuna pesa za TANESCO ambazo lazima zirudi kwa kiasi kilichopunguzwa. Bahati mbaya miaka saba baadae halikuwa limefanyika. 

Kama katika fedha hizo ipo kodi ya serikali, kwa mujibu kulikua na kodi ya ongezeko la thamani ambayo haikulipwa, IPTL hawakuilipa na uthamini ulikua bilioni 21 na ushee, TRA imepeleka madai yake kwa PAP.

CAG aliwaelekeza TANESCO kuacha kuhesabu pesa walizolipa kwenye akaunti ya escrow kama pesa zao, pesa hazikufikia sifa kuhesabika kama mali ya TANESCO(Asset). Mahakama kuu ya Tanzania ilifanya uamuzi katika shauri la maombi ya VIP, kusimamisha mchakato wa ufilisi wa IPTL na mahakama ikakubali.

Mfilisi aliagizwa kuhamisha kwa PAP kutoka IPTL ikiwemo akaunti escrow, ilizua mjadala mkali. Wizara ya nishati ilimwandikia mwanasheria mkuu kuomba ushauri, Mwanasheria akasema lipeni, uamuzi uko sawa na hauna matatizo na benki kuu wakauliza maswali hayo hayo na majibu yakawa yaleyale. Kuzingatia ushauri huo akaunti ikafungwa na pesa kukabidhiwa PAP. Mjadala ukaendelea bunguni na kwenye mablogu.

Na hata TANESCO alipewa ushauri huo huo, uamuzi ule umetiliwa shaka na kuonekana haukuwa sahihi na umeitia hasara nchi. Ukaibua hisia na ni kwa sababu nzuri tu kwamba si bure na iko namna kama ya rushwa na watu kunufaika binafsi. Mara kuna watu wameenda benki na kubeba pesa kwenye sandarusi, lumbesa na mengineyo.

Jambo moja ambalo ni bahati mbaya, ilijengeka dhana kuwa akaunti kufungwa ni jambo lililoanzishwa na maafisa wa serikali kwa manufaa yao binafsi.

Nilipokutana na mwanasheria mkuu, alisema hakukosea katika ushauri wake na wala mahakama haikufanya makosa, 

Na kuhusu ile hasara amesema hakuna hasara yyte iliyopatikana kwa sababu pesa imelipwa kwa mtu halali. 

Kabla ya mzozo wa ukokotoaji TANESCO ilikuwa inailipa ITPL Moja kwa moja. Lakini hata ulipotokea mzozo bado IPTL haikuacha kupeleka madai na Tanesco haikuacha kulipa. Kuwepo kwa akaunti ya escrow haibadili mwenye fedha yake. 

Kwa upande wa kodi ya serikali ambazo hazikulipwa, AG alipoulizwa alisema hakuna kodi iliyochelewa kulipwa.

Mgogoro ni baina ya IPTL na TANESCO havyo uamuzi wa standard charted haukuweza kuingia, kwa vile haikuhusishwa, ilienda kuzuia maamuzi hayo.

Fedha zilizotoka imelipwa PAP, akitokea mtu ana madai, serikali mnaikinga vipi. Ingetokea mtu ana madai yoyote angepelekwa PAP kulingana na makubaliano. Kukawa kuna hoja kuwa hata PAP umiliki wake wa hisa 70% unatia mashaka kutoka Mechmar, lakini waliziuza kwanza kwa kampuni ya Uingereza ambayo yenyewe ndo ikaziuza PAP. Kampuni ilikua chini ya ufilisi na kwa mujibu wa taratibu huwezi kuuza ukiwa chini ya ufilisi, kwa mujibu wa taarifa sio kweli. 

Tulitaka kufanya uchunguzi sisi wenyewe na mamlaka zetu na taarifa zimeshakuja, tunazifanyia kazi. 

Kuna vitu vimetokea, kuna vilivyofanyika nje na taarifa hazikuja na sasa tunalaumiana, hivyo tunafanya uchunguzi na wote waliohusuka tunawahoji na mahakama kuu ipo kesi ya PAP kumiliki hisa za IPTL, ipo kesi ya uhalali wa PAP kupokea pesa za IPTL. Hatutaki kuwaingilia ila sisi tutafanya uchunguzi wetu kwa ajili ya taarifa zetu. Tuwe na uhakika hizi hisa zimeuzwa kwa bei gani, tunataka kujiridhisha kwa sababu ipo kodi ya serikali(capital gain) na inalipwa na alieuza na sio alieuziwa. Kodi hulipwa na aliepata na sio aliepoteza(Alienunua). 

VIP walipouza na kupata dola milioni 78, wamelipa kodi bilioni 38. Kulikua na tuhuma za rushwa katika mchakato mzima. Yamesemwa mengi na bado hatujamaliza kuyasoma, rushwa ni kosa la jinai. Nilielekeza taarifa walizozipata wazipeleke PCCB. Nimeambiwa wanaendelea na mchakato wao. Kwa miamala, serikali inashughulika na watumishi wa umma kwa mujibu wa taratibu, maaskofu na masheikh kupewa kitu hawatuhusu, mtumishi wa umma ana masharti ya kupokea fedha. Watahojiwa na PCCB.

Hushtuki asubuhi akaunti ina bilioni 1.6, milioni 80 etc. Zimeanguka kutoka juu ya mti. Huo ndo utanguliza.

Maazimio ya bunge
Kwanza niseme serikali imayakubali na niwapongeze waheshimiwa wabunge. Nashukuru kamati ya bunge chini ya Zitto na Filikunjombe, watu wa upinzani kufanya yale maamuzi yao, kwamba CCM ni mafisadi. Ni kweli watu hawa wanatoka CCM ila sio kwamba CCM inaridhia. Ntashangaa mbunge kulipinga hili eti kisa tu yuko CCM, bunge wengi ni CCM, kama ni kweli walikuwa hawataki hakuna azimio lingepita? Na kuna baadhi ya wabunge wa CCM waliudhika na maovu haya, wenzetu wanatafuta sifa laini kwa jambo ambalo ni letu sote.

Niwahakikishie mimi na wenzangu serikalini hatuna upungufu wa dhamira katika kutimiza maazimio ya bunge.
Kutaifisha mitambo ya IPTL, tunahimiza sekta binafsi kuwekeza, tunapotaifisha habari tunayopeleka si nzuri, sisi tuliotaifisha mwanzo siku hizi tunasema hatuna sera ya ujamaa hivyo waje kuwekeza. Watasema wale jamaa wamerudia tena wanataifisha. Mahakama imefanya maamuzi kwa IPTL, kwanza waibadili mitambo yao ibadili itumie gas badala ya mafuta, tukiyafatilia yanaweza kutufikisha mahali. Haya ya kutaifisha yananipa wasiwasi

Kuhusu uwazi wa mikataba na mapitio, tutafanya na lipo moja tutafanya kuhusu usiri wao wa biashara, kuweka wazi zinaweza kutumiwa na wapinzani wa kibiashara, hivyo tutaangalia namna ya kulifanya. 

TAKUKURU na jeshi la usalama vichukue hatua, nimeshaeleza hatua zinaendelea.

Kamati za bunge kuwavua nyadhifa wenyeviti wa kamati za bunge

Raisi aunde tume ya kijaji kuwachunguza majaji(Mujulizi na Lwangisa), nimelipokea lakini utaratibu wa kisheria kushughulikia linatakiwa lianzie kwenye mahakama na sio linaanzia kwa rais au bunge. Mahakama inaporidhika amepoteza sifa, inaletwa kwa rais maana ndie anaeteua majaji. Lazima kushirikiana na muhumili wenyewe. Nilichosema tumwachie jaji mkuu na wakiridhika watakuja kwa raisi endapo wataridhika wahusika wamekosa sifa.

Kuhusu mabenki kuwekwa kama zinatakatisha fedha, pendekezo uchunguzi ufanyike ni pendekezo zuri na intelligence unit ndio watakaofatilia

Serikali iandae muswada wa sheria ulioleta TAKUKURU, ni wazo zuri, Mchakato wa kufanya mageuzi TAKUKURU tumeuanza tangu 2008. Sheria ya kwanza ya PCCB ilikua na makosa manne tu ya rushwa tukayaongeza mpaka 24.

Kuhusu watu kuwawajibisha, bodi ya TANESCO bahati nzuri imemaliza muda wake na tumeanza mchakato wa bodi, na tutaipata siku chache zijazo.

Katibu mkuu wa wizara ni mtumishi wa umma, hivyo kuna taratibu na nimeshaagiza zianze.

Mwanasheria mkuu wa serikali ameshajiuzulu na amesema amebeba dhamana hio pia kwa niaba ya waliojiuzulu.

Waziri wa ardhi, tumekaa nae na kuzungumza. Pesa hizi ni za nini na kwa ajili gani na amesema ni za shule, mengi yameelezwa. Maswali makubwa kwa nini hazijaenda shuleni moja kwa moja na zikawa kwa jina lake, akasema ndo masharti ya mtoaji, tumelitafakari sana na tumeona msingi mkubwa wa kimaadili kuhusu kupokea hizi pesa,tumeshazungumza nae na tumemwambia atupe nafasi tumteue mwingine.

Waziri wa nishati na madini tumemuweka kiporo, kuna uchunguzi nimeagiza ufanywe na nikipata majibu nitafanya uamuzi, tume ya maadili pia wanafanya kwa ajili ya kupata maamuzi kwa misingi ya haki.

NDIO MWANZO NA MWISHO WA HOTUBA YANGU NDEFU

Friday 19 December 2014

Mfahamu mzee mwenye wake 6,watoto 57 wajukuu 200 na vituku 70.

Mzee Nterege Nyigana Mutari ana umri wa miaka 103 ni mtu ambaye ni wapekee na alitahili kuwekwa katika kitabu cha maajabu duniani sababu amevunja rekodi kwa kuwa na watoto 57, wajukuu 200 na vituku 70.
hivyo kama hiyo haitoshi, unaamua kujenga shule
ili wapate elimu bora, tena katika shule hiyo
yenye wanafunzi 744, wanafunzi 200 wanatoka
katika familia yake, wakiwemo wajukuu na
vitukuu. Sasa mzee kama huyu, kwanini
asiwemo katika maajabu ya dunia?
Baada ya kufikiria mambo.
mengi.
Mzee Nterege ambaye ni mkazi wa
kitongoji cha Nyamaitagi, kijiji cha Nyamakobiti,
kata ya Majimoto Wilaya ya Serengeti mkoani ni wa kabila la
Wangoreme anaishi umbali wa kilometa 70
kutoka makao makuu ya wilaya ya Serengeti,
mjini Mgumu.

Historia ya Mzee huyo imejaa mengi yakiwemo
machungu na raha, lakini kwa upande wake
anasema vikwazo katika maisha ni jambo la
kawaida.
"Nina miaka 103, wajukuu zaidi ya 200 na
vitukuu zaidi ya 70, nilizaa watoto 57 lakini
ninachoweza kuieleza jamii ni kwamba watoto
wangu nimeamua kuwapa elimu bora kwa kuwa
elimu ndiyo ufunguo wa kila kitu hapa duniani,"
anasema Nterege.
Maisha yake
Nterege alizaliwa mwaka 1908 lakini akajulikana
kwa jina la "Reterenge'', jina ambalo anasema
alipewa na daktari raia wa Ujerumani.
Anasema alizaliwa katika eneo la Kyehonda -
Kimeli ambalo kwa sasa ni eneo la kijiji cha
Nyamutita na kwamba wakati huo baba yake
alikuwa na wake wawili.
"Kwa upande wa mama yangu tulizaliwa wawili
tu, mimi na dada yangu ambaye anaitwa
Nyakimaiga, mama yetu alikuwa mke wa pili wa
baba," anasema Nterege.
Anasema mwaka 1918 baada ya baba yake
kufariki dunia, ndugu wa baba yake walichukua
mifugo yote iliyoachwa na baba yake wakiwemo
Ng'ombe zaidi ya 100, na kuwanyang'anya
nyumba waliyokuwa wakiishi na mama yao.
"Walitufukuza pamoja na mama kwa kuwa
alikuwa mke mdogo wa marehemu baba,
walisema kuwa mama yetu wa kambo ambaye
alikuwa mke mkubwa ndio alikuwa na haki ya
kupata kila kitu. Kuanzia hapo tulianza kuishi
kwa shida."
Anasema baada ya tukio hilo alianza maisha ya
kujitegemea ambayo yalimfanya ashindwe
kwenda shule na kujikita katika kilimo na wakati
mwingine kufanya kazi ya kuchunga mifugo ya
watu mbalimbali ili kupata fedha za kuweza
kujikimu.
"Mwaka 1937 nilioa mke wa kwanza, Wansama
Moremi ambaye kwa sasa ni marehemu nilihamia
eneo la Nyamakobiti kuanza maisha mapya ya
ndoa…, mke wangu nilimtolea maali ya Ng'ombe
kumi niliowanunua baada ya kuuza Ulezi
niliolima kati ya mwaka 1935 na 1936," anasema
Nterege.
Wazo la kuwa na familia kubwa
Anasema katika maisha yake mapya baadhi ya
mambo yaliyokuwa yanamsumbua, ilikuwa ni
jinsi gani angeweza kupata watoto wengi kwa
kuwa alizaliwa yeye na dada yake tu.
"Wakati ule kuwa na familia au ukoo mkubwa
kilikuwa kitu cha heshima katika mila zetu,"
anasema Nterege.
Pia, anasema ukubwa wa familia ulikuwa
muhimu ili kuweza kupambana na vitendo vya
wizi wa mifugo ambapo mara kwa mara
kuliibuka mapigano ya kikabila kati ya kabila
lake na Wakulya na Wangoreme.
"Maisha ni mapambano. Nilianza kufanya
biashara ya mifugo mwaka 1940 nikishirikiana
na Chifu Makongoro wa Waikizu. Nilipata
Ng'ombe 800 wa kwangu mwenyewe ila kwa
sasa wamebaki 220 baada ya kuwapa watoto
wangu kwa ajili ya kuanza maiasha yao ya
kujitegemea,"
Kuoa
Akizungumza wanawake aliowaoa Nterege
anasema,
"Nilioa wanawake saba lakini niliodumu nao ni
sita, wanawake hao sita walizaa watoto 57, ila
watoto waliopo hai ni 37,".
Anaongeza, "Watoto wangu 20 walifariki
kutokana na kwamba wakati huo vituo vya kutoa
huduma ya afya vilikuwa mbali,".
Anasema kuwa ana wajukuu zaidi ya 200,
vitukuu zaidi ya 70 na anafafanua ," Wengine
siwatambui hata kwa majina,".
Anasema mwaka 1937 alimuoa mke wake wa
kwanza, Wansama Moremi, Gasawa Mayengo
(1939),Mandala mwita (1953), Nyamhanga
Nyamani (1963), Odela Osole (1969), Nyambura
Paka (1965) na Mkami Myangosira (1974)
ambaye waliachana bila kuzaa mtoto.
Anasema mpaka sasa wake zake walio hai ni
wawili ambao anaishi nao na anawataja kuwa ni
Nyamhanga Nyamani na Nyambura Paka.
Nterege anasema jambo kubwa analojivunia ni
kumwona mtoto wake wa mwisho, Julius
akisoma elimu ya sekondari ambapo alimaliza
mwaka juzi.
Anasema kaka yake Julius anayeitwa Nyamanko
alimaliza sekondari mwaka 1990, na wajukuu
zake watano nao wamemaliza elimu ya
sekondari ambao ni Gesile(2003), Bonifasi
(2009), Nyakimaiga (2011).
"Kuna mmoja anaitwa Nyamitari bado yupo
kidato cha tatu kwenye shule ya Sekondari ya
Busawe, shule ambayo nilichangia ujenzi wake,"
anaeleza kwa kujivunia kwa kitendo chake cha
kuchangia maendeleo ya jamiii.
Anasema watoto wake 19 ambao wako hai ni wa
kike na wa kiume 18. Mtoto wake wa kwanza
anaitwa Mayengo na alizaliwa mwaka 1942.
Kujenga shule
Mzee Nterege ambaye bado ana kumbukumbu ya
mambo mengi licha ya kuwa na umri mkubwa
anasema kuwa mwaka 1988 baada ya kuona
wajukuu zake wakipata usumbufu wa kwenda
shule zilizokuwa vijiji vya mbali, aliamua kubuni
wazo la kuanzisha shule ya msingi kuondoa
usumbufu huo.
Anasema alianza ujenzi wa shule kwa kutumia
magari yake kubeba mchanga na kokoto huku
akiwahamasisha wakazi wa kijiji hicho kuchangia
ujenzi.
"Ilikuwa ngumu kuwashawishi kwa kuwa kipindi
hicho watu walikuwa hawapendi kuelezwa habari
za kuchangia fedha kwa ajili ya jambo fulani.
Anasema kwamba mwaka 1990 alifanikiwa
kumaliza ujenzi wa jengo la utawala kwa nguvu
zake pamoja na wananchi.
"Licha ya kuwa mimi sikusoma niliamua kujenga
shule ili wajukuu zangu wapate elimu. Elimu
ndiyo kila kitu. Huwezi kufanikiwa katika maisha
ya sasa bila elimu. Niliona wajukuu zangu
wasiposoma watakuwa watumwa na tegemezi,"
anaeleza Nterege.
Anasema mwaka 1991 shule hiyo ya msingi
iliyopewa jina la Nayamakobiti ilifunguliwa kwa
usajili namba PS 0904080 ikiwa na eneo la
ukubwa wa Hekta 9.5.
"Shule hii niliamua kuiita jina la kijiji badala ya
jina langu kwa kuwa sikutaka sifa katika suala
hili, mtu unatakiwa usifiwe ukiwa umekufa si
ukiwa hai," anasema Nterege.
Mkuu wa shule hiyo anasemaje
Akizungumzia historia ya shule hiyo mkuu wa
shule hiyo, Machumbe Mairo anasema kuwa
huwezi kuzungumzia maendeleo ya shule hiyo
bila kumtaja mzee Nterege.
Anasema shule hiyo ina wanafunzi 744 na
anafafanua kwamba pamoja na changamoto
zinazoikabili shule hiyo ikiwa ni pamoja na
uhaba wa walimu.
Pamoja na matatizo hayo alisema inafanya vizuri
ambapo wanafunzi wengi hufaulu kuendelea
kidato cha kwanza.
"Katika kipindi cha mwaka 2006 hadi 2010 shule
hii imeweza kufaulisha wanafunzi 122 kwenda
sekondari, wasichana wakiwa ni 41 na 81
wakiwa ni wavulana," anasema Mairo.
Anasema wanafunzi 200 wa shule hiyo kati ya
wanafunzi 744 wanatokea katika familia ya mzee
Nterenge wa kiwemo wajukuu na vitukuu.
"Familia yake ni kubwa kweli yaani hapa kijijini
wako wengi. Ukienda vijiji jirani pia wapo,"
anasema .
Chanzo:MWANANCHI.

IPTL na PAP pamoja na Harbinder Singh Seth wafungua kesi

KAMPUNI za Pan Africa Power Solution
Tanzania Limited (PAP) na Independent
Power Tanzania Ltd (IPTL) na Harbinder
Singh Sethi, wamefungua kesi ya kikatiba
kupinga utekelezaji wa maazimio ya Bunge
yaliyotolewa kuhusu sakata la Akaunti ya
Tegeta Escrow katika Benki Kuu ya Tanzania
(BoT), inayodaiwa kuchotwa zaidi ya Sh
bilioni 300.
Kesi hiyo ilifunguliwa jana katika Mahakama
Kuu Kanda ya Dar es Salaam chini ya hati
ya dharura dhidi ya Waziri Mkuu, Mkurugenzi
Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana
na Rushwa (Takukuru), Spika wa Bunge na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Ilifunguliwa kupitia mawakili watatu wa
kampuni hizo, ambao ni Joseph Makandege,
Melchsedeck Lutema na Gabriel Mnyele.
Mawakili hao wanadai kwamba uamuzi
uliotolewa na Bunge, uliegemea upande
mmoja kwa vile baadhi ya wahusika
walioshiriki, ikiwamo Mbunge wa Kigoma
Kaskazini, Kabwe Zitto na Mbunge wa
Kigoma Kusini, David Kafulila wana kesi
kuhusu sakata hilo.
Pia, walidai kilichofanyika ndani ya Bunge
kuhusu sakata hilo ni kinyume cha Katiba
kwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria
alitafsiri vibaya amri halali, iliyotolewa na
Mahakama ya kuzuia mjadala huo usijadiliwe
bungeni.
Mawakili hao walidai kwamba mahakama
ilikusudia Bunge liweze kuendelea na
shughuli zake za kawaida wakati shughuli
nyingine zinazohusu maombi hayo
zikitekelezwa.
Miongoni mwa maazimio yaliyowasilishwa
bungeni ni kwamba Sethi, James Rugemalira,
Waziri wa Nishati na Madini na Katibu Mkuu
wake, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),
walihusika kufanya miamala haramu ya
fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow kwenda
kwa makampuni ya PAP na VIP Engineering
& Marketing.
Bunge liliazimia kwamba Takukuru, Jeshi la
Polisi na vyombo vingine husika vya ulinzi na
usalama, viwachukulie hatua stahiki za
kisheria, kwa mujibu wa sheria za nchi, watu
wote waliotajwa na Taarifa Maalum ya
Kamati kuhusika na vitendo vyote vya kijinai
kuhusu miamala ya Akaunti ya Escrow.
Pia, bunge lilisema kutokana na vitendo vya
kijinai wanavyohusishwa navyo viongozi wa
umma na maofisa wa ngazi za juu serikalini,
vinakiuka maadili na kuwanyima viongozi na
maofisa hao uhalali wa kuendelea kushikilia
nafasi za mamlaka katika uongozi wa umma
wa kuwawajibisha kwa kuishauri.
Hivyo azimio la pili Bunge liliwataka viongozi
hao akiwemo Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, wawajibishwe, kwa
kuishauri mamlaka yao ya uteuzi kutengua
uteuzi wao.
Katika azimio la tatu, Bunge liliazimia
kwamba Kamati za Bunge zichukue hatua za
haraka, kwa vyovyote kabla ya Mkutano wa
Kumi na Nane wa Bunge, kuwavua nyadhifa
zao Wenyeviti tajwa wa Kamati husika za
Kudumu za Bunge; Pia, azimio la nne, Bunge
lilimtaka Rais Jakaya Kikwete aunde Tume
ya Kijaji ya Uchunguzi, kuchunguza tuhuma
za utovu wa maadili dhidi ya Jaji Aloysius
Mujulizi na Jaji Profesa Eudes Ruhangisa wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, ambao
wanahusishwa katika kashfa hiyo.
Maazimio mengine yaliyotolewa na Bunge
kuhusu sakata hilo ni mamlaka husika za
kifedha na za kiuchunguzi, ziitaje Stanbic
Bank Ltd na benki nyingine
zitakazogundulika, kufuatia uchunguzi
uliofanywa na mamlaka za kiuchunguzi,
kujihusisha na utakatishaji wa fedha
zilizotolewa katika Akaunti ya Escrow, kuwa
ni taasisi zenye shaka ya utakatishaji wa
fedha haramu.
Hata hivyo, Bunge liliitaka Serikali iandae na
kuwasilisha Muswada wa marekebisho ya
Sheria iliyoiunda Takukuru kwa lengo la
kuanzisha taasisi mahsusi
itakayoshughulikia, kupambana na kudhibiti
vitendo vya rushwa kubwa, ufisadi na
hujuma za uchumi zinazotishia uhai wa taifa
kiuchumi, kijamii na kisiasa; Vile vile, Bunge
liliaazimia kwamba Serikali iangalie
uwezekano wa kununua mitambo ya kufua
umeme ya IPTL na kuimilikisha kwa Tanesco
kwa lengo la kuokoa fedha za Shirika hilo.
chanzo cha habari hii gazeti#habari leo

Friday 5 December 2014

Waishi na maiti miezi 6



Familia moja nchini Canada iliishi na maiti katika chumba cha juu cha nyumba yao kwa miezi sita kwa kuwa waliamini marehemu atafufuka iwapo wataendelea kumuomba mungu,lakini mwili huo ukapatikana baada ya familia hiyo kushindwa kulipa mkopo waliochukua kununua nyumba hiyo.
Kaling Wald mwenye umri wa miaka 50 alipatikana na makosa ya kushindwa kuwaarifu maafisa wa polisi kwamba mumewe alifariki ,kosa ambalo na akahukumiwa kuwekwa katika muda wa majaribio na ushauri,wakili wake alikiambia chombo cha habari cha Reuter siku ya Jumanne.
Peter Wald mwenye umri wa miaka 52 alifariki mnamo mwezi machi mwaka 2013 kwa kile mamlaka inasema ni sababu za kawaida kufuatia maambukizi ya mguu wake yanayodaiwa kusababishwa na ugonjwa wa sukari.
Mkewe Kaling Wald alimwacha kitandani na kufunga chumba hicho katika nyumba yao ya Hamilton ,Ontario ili kuzuia harufu kali iliokuwa ikitoka chumbani humo kuwafikia watu waliokuwa wakiishi nyumbani humo.
Kama vile Yesu alivyomfufua Lazaro baada ya siku ya nne ,pia yeye aliamini kwamba Mungu atamfufua mumewe wakili wa mwanamke huyo alisema.

ICC imetupilia mbali kesi ya jinai inayokuwa inamkabili Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.



Mwendesha mkuu wa mashitaka Fatou Bensouda ameondoa kesi dhidi ya Kenyatta ambaye alidaiwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007/2008.
Mahakama ilikuwa imempa Bensouda wiki moja kuamua ikiwa ataendelea na kesi dhidi ya Kenyatta au la inagwa alisema muda huo haukutosha kwake yeye kuandaa ushahidi zaidi dhidi ya Kenyatta.
Kenyatta alishtakiwa kama mshukiwa mkuu wa ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007/2008 akituhimiwa pamoja na William Ruto ambaye ni naibu Rais kwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu.
Zaidi ya watu elfu moja waliuawa wakati wa ghasia hizo. Uhuru alikuwa mtu maarufu zaidi kufikishwa mahakamani na pia mshukiwa mkuu kwani alifikishw amahakamani akiwa Rais aliye mamlakani.
Hili ni pigo kubwa kwa upande wa mashitaka, wengi wlaioana keshi dhidi ya Kenyatta kama mtihani mkubwa katika historia ya mahakama hio.
Upande wa mashitaka ulitaka mahakama kuupatia muda zaidi ili upate ushahidi zaidi,dhidi ya Kenyatta kama vile taarifa za akaunti yake ya benki.
Upande wa utetezi uliteta kuwa ikiwa hakuna ushahidi wa kutosha kesi hio inapaswa kutupiliwa mbali.

Tekinolojia mpya ya Simu yagunguliwa..


Tuesday 2 December 2014

Mbinu za mafanikio katika biashara

Mbinu katka biashara yako ili kufanikiwa  inakubidi uwe na jitihada za ziada.
Kadiri mtu anavyoongeza jitihada katika usimamizi wa biashara yake, ndivyo anavyopata mafanikio.
Inapaswa kutumia jitihada za kiakili na kimwili.
Watu wengi huanza biashara baada ya kuchoka kutokana na kufanya kazi aliyoajiriwa kwa muda mrefu au kupata ‘presha’ kutoka kwa bosi wake ofisini.
Hivyo fikra kubwa aliyonayo ni kwamba katika biashara yake anakwenda kupumzika kwa kuwa ana wasaidizi, kazi yake itakuwa ni kusaini hundi tu.
Mwisho anakuja kushtukia hakuna biashara inayoendelea kwa kuwa hakuonesha jitihada tokea mwanzo.
Kumbuka kuwa kufanya biashara si jambo rahisi, linahitaji nidhamu ya hali ya juu katika utendaji kazi.
Uanzishwaji na ukuaji wa biashara unahitaji muda mwingi zaidi ya wengi wanavyodhani.
Hapo inabidi ufanye kazi muda mwingi, na kubakia na fedha kidogo za matumizi ya nyumbani, hadi pale biashara yako itakapoimarika.
Biashara inahitaji nidhamu ya hali ya juu, hata kama hakuna mtu anayekufuatilia au kukuonya pale unapokosea.
Inakupasa kuwa kwenye biashara yako kama ulivyojipangia ratiba yako ya kila siku.
Watu watakuwa wanakutafuta, pale wanapokuhitaji inabidi wajue unapatikana muda gani, unapokosekana unawavunja moyo wateja wako na kukosa fursa ambazo zingekupatia faida.
Pia inakubidi kutumia muda wa ziada na rasilimali zaidi endapo mauzo yako hayaendi vizuri.
Fanya soko au biashara yako ionekane kwa wateja wako.
Pia ni vizuri katika biashara unayoifanya, isihusishwe na familia yako. Hapa inamaanisha hata kama unafanya biashara, endapo mwanafamilia atahitaji kitu itambidi akinunue sio kuchukua bure.
Kuruhusu biashara yako iwe holela kwa familia, kutafanya ifilisike baada ya muda mfupi.
Ni vema kuweka muongozo mzuri kwa familia yako ili jambo hili liendelee.
Ushauri mwingine ni kwamba, ili biashara yako isonge mbele inakubidi uwe mvumilivu.
Ni kawaida biashara yoyote haiwezi kukua kwa siku moja. Inachukua muda kueleweka kwenye soko, kukubalika na wateja na kuweka mtandao safi.
Inabidi uwe imara katika malengo uliyojiwekea katika kipindi kigumu utakachokipitia.
Biashara nzuri ni kama miti mizuri inayochukua muda kukua. Lakini pale inapokuwa inastahimili kimbunga cha aina yoyote.
Na kama unaijenga biashara yako katika eneo lenye misukosuko ya kibiashara inakubidi uandae msingi imara unaohitaji uvumilivu.

Picha 9 Hotel chini ya maji TZ

Hotel ya kifahari chini ya maji imezinduliwa hivi karibuni inajulikana kama Mantal Resort ipo visiwani Pemba zanzibar nchini Tanzania.

Mantal Hotel imekuwa gumzo katika vyombo vya habari kwani ndio hotel yenye vyumba 16 ndani ya maji barani Africa.

 Hii hotel  vyumba vyake vipo chini ya maji na ukiwa chumbani kupitia dirishani unaweza kuwaona samaki wa kila aina wakipita wakiwa wanaogelea wala hawana madhara yeyote kwa mtu kwani ni sehemu salama kabisa.

Bei ya kulala kwa siku moja single ni $900 zaidi ya million moja ya kitanzania na double ni $1500 zaidi ya milion mbili pia za kitanzania na. Manta Resort imekuwa designed by Swedish company Genberg Underwater Hotels kwa mujibu wa CNN.

HIZI NI PICHA ZA MANTA RESORT