Pages

Monday 22 August 2016

Mtu mmoja ameza visu 40 nchini India

MTU  mmoja nchini India afanyiwa upasuaji  kuondoa visu tumboni ambavyo amelivimeza ndani ya miezi miwili na kufikia visu 40.

Kwa mujibu wa daktari ambaye aliongoza operesheni alisema inasemekana mgojwa huyo kumeza visu ilikuwa ni tabia yake sugu kwa kuwa alikuwa anameza visu hivyo kwa siri bila hata familia yake kujua,

Hata sisi Madaktari tuliobobea katika fani hii tulipata changamoto katika kufanya upasuaji huo "Dk.Jatinder Malhotra aliiambia CNN.

Dr.Malhotra alisema mgojwa huyo mwanamme mwenye umri wa miaka 42 aliwashukuru madaktari kunusuru maisha yake pia aliomba msamaha familia yake.



Lakini swali kubwa aliloulizwa "kwa nini  kuanza kula visu? "Hata mimi sijui ni kwa nini Nilikuwa nakula visu, Lakini ilikuwa starehe nilipenda ladha yake nikawa addicted(muhanga) ... kama jinsi watu wanavyokuwa addicted na pombe na mambo mengine, hali yangu ilikuwa ni sawa" mgonjwa aliiambia CNN.

No comments:

Post a Comment