Pages

Sunday 27 March 2016

TIMU YA CHAD YAJIENGUA AFCON 2017

Timu ya Taifa ya Chad 'Les Sao' imejiondoa katika michuano ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika (AFCON) itakayofanyika mwaka 2017 nchini Gabon.

Taarifa ya kujitoa kwa Chad imetolewa na Shirikisho la Mpira wa miguu barani Afrika (CAF) leo baada ya Les Sao kuandika barua ya kujitoa katika mashindano hayo ikiwa katika kundi G pamoja na timu za Tanzania, Nigeria na Misri.

Chad ilitarajiwa kucheza Leo Jumatatu dhidi ya Tanzania katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, ikiwa ni mchezo wa marudiano wa kundi G baada ya kucheza mchezo wa awali jijini N'Djamena katika ya wiki.

Katika mchezo wa awali uliochezwa uwanja wa Idriss Mahamat Ouya, Taifa Taifa Stars ingecheza mchezo wake wa pili wa marudiano na Chad leo Jumatatu ya March 28 uwanja wa Taifa Dar Es Salaam , baada ya mchezo wa kwanza kufanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0.

No comments:

Post a Comment