Pages

Saturday 29 August 2015

Baadhi ya Vipaumbele vya ilani ya UKAWA viko hapa.

Mkutano mkubwa wa uzinduzi wa ufunguzi wa kampeni za vyama vya upinzani umoja wa katiba (UKAWA)umevunja rekodi kwa kuwa kukusanya maelfu ya wanachama toka pande zote za nchi katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya jangwani jijini Dar es salaam..
Katika mkutano huo ukawa wamezindua ilani ya kampeni zao ambapo mh. Edward Lowassa ambae ni mgombea urais wa ukawa alipo pewa nafasi ya kuhutubia amesema wantanzania wampigie kura ili afanye mabadiliko.
Lowassa ametaja baadhi ya vipaumbele katika ila ya ukawa watafanya mabadiliko katika elimu kwa kutoa elimu bure kuanzia shule ya msingi mpaka chuo kikuu.
Kwa upande wa afya ukawa watatoa kipaumbele katika afya ya mama na watoto kwa kuwa ndio wahanga wakubwa katika sekita hii na mama ndio msingi wa taifa lolote duniani kwani kila mtu kazaliwa na mwanamke.
Amemalizia kwa kusema atahakikisha sekita ya usafiri inaboreshwa kwa kufufua usafiri wa ndege hususani ikiwa ni kuifufua Air tanzania.
Aidha kwa upande mwingine mh. Lowassa amemalizia kwa kuahidi wananchi wakimchagua na akawa raisi atawatoa jera mashehe na watu wengine waliopo gerezani ikiwa ni pamoja na mwanamuziki mashuri hapa nchi Babu Seya.



No comments:

Post a Comment