Pages

Wednesday 26 August 2015

Ujue Ugojwa Hatari wa Kipindupindu.

Kipindupindu ni ugonjwa hatari wa mlipuko unaosababishwa na bakteria ajulikanaye vibrio cholera hushambulia mwilini hasa katika utumbo mwembamba baada ya hapo mgojwa huanza kuhara majimaji yenye rangi kama maji ya kupikia mchele pamoja na kutapika na homa kali.

Kiwango cha kutapika sana kinaleta upungufu wa maji mwilini na kupelekea kutokuwepo na uwiano wa chumvi mwilini na huweza kupelekea mgojwa kufariki iwapo atacheleweshwa kupatiwa tiba.

Kipindupindu hutokea iwapo mgonjwa akitumia maji yasiyo safi na salama kwa kunywa.

Bakteria anayesabisha kipindupindu (vibrio cholerae) hupatikana hasa katika maji yaliyochanyika na kinyesi cha binadami na maji ya chooni.

Inashauriwa ili kujikinga kutopata maambikizi ya ugonjwa huu ni kuhakikisha unakunywa maji safi na salama yaliyochemushwa na wakati wowote kunawa mikono kabla ya kutayarisha au kula chakula,kusafisha vyombo kama sahani,vikombe.
 unaponawa mikono hakikisha unanawa na sabuni kiganjani upande wa nyuma wa mkono, katikati ya vidole na kucha kwa sekunde.Baada ya kutoka chooni na kabla ya kula chakula na matunda kusafishwa vizuri na maji yaliyochemshwa.

Mgonjwa wa kipindupindu huweza kupatiwa matibabu huku lengo kuu likiwa ni kurejesha maji na madini mwilini aliyoyatoa kwa njia ya kuhara au kutapika.
Njia itumikayo kumpatia maji hayo ni kwanjia ya mdomo ambapo hupewa anywe au kwanjia ya mshipa wa damu ambayo kitaalamu hujulikana kama intravenously(i.v),Mgonjwa hunyweshwa maji mengi, kwa sababu mwili wake hupoteza maji mengi anapougua maradhi haya kwa njia ya kuhara na kutapika na Dawa zinazojulikana kufanya kazi ni kama cotrimoxazole, erythromycin, doxycycline, chloramphenicol, na furazolidone.

No comments:

Post a Comment