Pages

Sunday 30 August 2015

Daktari Bingwa toka Tanzania atwaa Tuzo Uingereza.

Daktari Bigwa mshauri wa maradhi ya Moyo Dr.Harun Elmada Nyangori kutoka Hospitali ya Rufaa Morogoro hapa nchini awa mtanzania wa kwanza kupewa tuzo ya kimataifa na kutambuliwa na Baraza la Madaktari Bingwa wa Shirikisho la nchi za Ulaya (uropean Society of Cardiology).

Akitoa tuzo hiyo ya heshima kwa Dr.Nyangori Rais wa shirika hilo prof. Pinto alisema Tanzania imekuwa nchi ya pekee kuweka historia kushiriki katika mashindano ya kutoa mada za utafiti wa maradhi ya moyo.
Hivyo Dr . Nyagori amekuwa Daktari wa kwanza kushiriki na kuwa chachu ya kufungua mlango kwa madaktari wengine wajitokeze kufanya tafiti mbalimbali zinazohusu taaluma ya magojwa ya Moyo.

No comments:

Post a Comment