Pages

Wednesday 16 September 2015

Jk ateua katibu wa Tume ya kurekebisha Sheria

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Ndugu Casmir Kyuki kuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria.


Kabla ya uteuzi huu, ndugu Kyuki alikuwa Mwandishi Kufuatia uteuzi huu, Rais amemteua Bibi Sarah Barahomoka kuwa Mwandishi Mkuu wa Sheria, kujaza nafasi iliyoachwa wazi na ndugu Kyuki.

Kabla ya uteuzi huu, Bibi Barahomoka alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya uandishi wa Sheria. Uteuzi huu unaanza mara moja.

Wateule hawa wataapishwa Tarehe 16 Septemba, 2015, Ikulu Dar-es-Salaam leo saa 3 asubuhi.


Imetolewa na:

Premi Kibanga,

Mwandishi wa Habari, Msaidizi,

Ikulu-DSM

15 Septemba, 2015

No comments:

Post a Comment