Pages

Sunday 20 September 2015

Mabasi ya Mwendo Kasi Mengine yawasili Dar

TATIZO la usafiri katika jiji la Dar es Salaam linatarajia kupungua kufuatia kuwasili kwa mabasi 138 katika Bandari ya Dar es Salaam kutoka China tayari kwa huduma ya usafiri. 


Msemaji wa Kampuni ya UDA Rapid Transit(UDA-RT),Bw,Subri Maburuki alisema mabasi yote yameingia yakiwemo ya mita 12 yapo 101 na mita 18 yapo 39 na huduma ya usafiri kipindi cha mipito itanza baada ya kukamlisha taratibu za bandari. 

 "Tuliahidi kuwa mwezi huu wa tisa mabasi yatakuwa yamewasili na ni kweli yamemekuja," na kwa pamoja na yale ya kufundishia yatakuwa jumla mabasi 140", alisema Bw. Maburuki na kufafanua kwamba mabasi hayo yametokea kiwandani China na yanakidhi miundombinu ya barabara ya mradi wa BRT kama walivyokubaliana. 

 Aidha Kaimu Meneja Bandari ya Dar es Salaam, Bw.Hebel Mhanga alisema meli iliyobeba mabasi hayo ilipitia Kenya na kimsingi ilitokea China ilikuwa imebeba magari 1700 yakiwemo mabasi ya UDA-RT. 

 "Hatua hii ni ya msingi kwa nchi yetu, itasaidia wakazi kusafiri kwa urahisi na haraka,"alisema Bw. Mhanga. UDA-RT ni kampuni iliyoundwa na wazalendo kwa ajili ya kutoa huduma ya usafiri katika barabara ya DART jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment